Katika siku za hivi karibuni,wito umetolewa wa kuwekwa kwa mikakati ya kukinga dunia dhidi ya mabadiliko ya tabia-nchi.
Wanasiasa wakuu ulimwenguni sasa wanadai kuwa iwapo hatukutakuwepo na hatua za haraka za kuzuia athari zaidi,huenda dunia ikakumbwa na tishio la usalama.Mmoja wa hao ni waziri wa maswala ya nje ya Ujerumani ambaye amesema ulimwengu unahitaji kufikiria mikakati zaidi kuzuia mabadiliko ya tabia-nchi.
Aidha,Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron pamoja na waziri Mkuu wa Uingereza,Boris Johnson wameungana na kusema kuwa dunia yafaa kulinda mazingira ili kuzuia ongezeko la joto duniani.
Ikumbukwe kuwa ulimwengu mzima umeshuhudia ongezeko la joto pamoja na kukauka kwa vidimbwi vya maji hivyo kuongeza migogoro kuhusu rasilimali chache zinazosalia.
Kumewepo na wito wa kupunguza matumizi ya gesi zinazochafua hewa na kuharibu utando wa ozoni.
Nchi kadhaa zimekuwa na ukosefu wa chakula kutokana na ukosefu wa maji ya kunyunyizia mimea shambani ili yakue.